Alhamisi, 30 Juni 2016

SIMBA SPORTS CLUB IMETHIBITISHA KUHUSU KOCHA MKUU WA TIMU HIYO


Klabu ya Simba Fc Imethibitisha rasmi kuwa mkameroon Joseph Omog kuwa ndiye kocha kuu wa timu hiyo.Lakini pia kocha huyo aliwah isaidia Azam Fc kupata ubingwa msimu wa 2013/2014.






Jumanne, 28 Juni 2016

TP MAZEMBE YAIKONG’OLI YANGA KAMOJA UWANJA WA TAIFA

index 
Mshambuliaji wa timu ya Yanga,Obrey Chirwa akiichambua ngome ya timu ya TP Mazembe, katika mtanange uliopigwa jioni hii kwenye dimba la Taifa (Uwanja wa Taifa) Jijini Dar es salaam, ikiwa ni Mchezo wa Kombe la Shirikisho Barani Afrika. Hadi kupanga cha mwisho kinalia, Yanga wamelala kwa bao 1-0.(Picha na michuziblog)
tai2  
Mashabiki wakiwa wamefurikwa kwenye uwanja wa Taifa hata hivyo mwishowe wakaondoka vichwa chini baada ya timu yao kupoteza mchezo huo mbele ya mahasimu wao TP Mazembe

SHAMO WORLD YATOA MSAADA KITUO CHA WATOTO YATIMA CHA MAUNGA JIJINI DAR LEO.

 Mwakilishi wa Kampuni ya Shamo World Foundtion, Salama akikabidhi baadhi ya Vitu vya msaada kwa  Mlezi Mkuu wa Kituo cha kulelea watoto yatima cha Maunga Centre, Zainabu Maunga jijini Dar es Salaam leo wakati walipotembelea katika kituo hicho kilichopo karibu na kituo cha Polisi cha Hananasif jijini Dar  es Salaam.
Akizungumza wakati wa kukabidhi msaada huo mwakilishi wa kampuni ya Shamo World Foundation amesema kuwa wameguswa kutoa msaada katika  kituo hicho kwa kutenda matendo ya huruma wakati wa kipindi hiki cha Mwezi wa Ramadhani kwa watoto kwa kuwa wanamahitiji mengi pia ni kuwapunguzia ugumu wa maisha walezi wa watoto hao.
 
Nae Mlezi Mkuu wa Kituo cha kulelea watoto yatima cha Maunga Centre, Zainabu Maunga amewashukuru kampuni ya Shamo World kuwaona kwa jicho la pekee na kwenda kuwapa msaada katika kituo hicho.
 
Mwakilishi wa Kampuni ya Shamo World Foundation, Salama amesema kampuni hiyo wamekabidhi Kg 50 za Mchele, Kg 50 za unga wa ngano na unga wa ugali, Kg 50 za sukari pamoja na Maboksi 15 ya Tende pamoja na mafuta ya kupikia.
 Wawakilishi wa Kampuni ya Shamo World Foundation, Salama  na Zaituni Ramadhani wakikabidhi mafuta ya kupikia kwa watoto kwa kituo cha kulelea watoto yatima cha Maunga jijini Dar es Salaam leo.
Wawakilishi wa Kampuni ya Shamo World Foundation, Salama  na Zaituni Ramadhani wakiwa katika picha ya pamoja na walezi wa kituo cha kulelea watoto yatima na watoto walio klatika kituo hicho jijini Dar es Salaam leo.

WIZARA YA ARDHI YAANZA KUTOA HUDUMA KATIKA MAONESHO YA SABASABA

MAB1 
Banda la maonesho la Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi likiwa limeanza rasmi kutoa huduma katika viwanja vya maonesho vya Mwalimu Nyerere vya Sabasaba Dar es salaam.
MAB2 
Baadhi ya Wananchi wakipata maelezo ya huduma za mipango miji zinazosimamiwa na Wizara ya Ardhi.
MAB3 Muoneshaji wa Wizara ya Ardhi bi. Mwanamkuu Ally akiwapa maelezo wananchi waliotembelea banda la Wizara ya Ardhi kifaa kinachotumika katika upimaji wa Ardhi cha aina ya Total station.

Tatizo la mikopo kupatiwa ufumbuzi

TANT1 
Wananchi mbalimbali wakiingia katika Maonyesho ya 40 ya Biashara ya Kimataifa yanayofanyika katika viwanja vya Mwalimu Nyerere barabara ya Kilwa kwa ajili ya kujipatia bidhaa mbalimbali.Maonyesho hayo yameanza leo hii Jijini Dar es salaam.Picha n Daudi Manongi,MAELEZO
TANT01 
Askari wa JKT pamoja na FFU wakihakikisha usalama wakati wananchi wakiingia katika viwanja vya Mwalimu Nyerere kuangalia bidhaa mbalimbali baada  ya maonyesho ya 40 ya Biashara ya Kimataifa kuanza leo jijini Dar es salaam.
TANT3 
Afisa Habari Idara ya Habari,MAELEZO Bi.Immaculate Makilika akizungumza jambo na Afisa Biashara kutoka Wizara ya Viwanda ,Biashara na Uwekezaji Bw.Baruti Mwaigaga(kushoto)  katika banda la Wizara hiyo viwanja vya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.
TANT4Mwananchi akiangalia moja ya bidhaa  zinazotengenezwa na kikundi cha African Flowerless fashion cha Arusha kinachouza bidhaa zake nje ya nchi.Kulia ni Afisa wa kikundi hicho Bi.Suzana Mwalongo.
TANT5 
Mafundi wakiendelea na upakaji rangi katika banda la CRDB katika Maonyesho ya 40 ya Biashara ya Kimataifa viwanja vya Mwalimu Nyerere jijini Dar e Salaam.
…………………………………………………………………………………
Na: Immaculate Makilika- MAELEZO, Dar es salaam.
SERIKALI kupitia Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji imeandaa mkakati ya kulipatia ufumbuzi tatizo la ukosefu wa mikopo linalowakabili wafanyabiashara wengi nchini ili kusaidia uanzishwaji wa viwanda.
Hayo yamesemwa na Afisa Biashara wa Wizara hiyo Bw. Baruti Mwaigaga wakati akizungumza katika Viwanja vya  Mwl Nyerere wakati wa maonesho ya Sabasaba yaliyoanza leo jijini Dar es Salaam.
“Kufuatia kuwepo kwa tatizo kubwa la upatikanaji wa mikopo kwa watu wenye nia ya kuanzisha viwanda hapa nchini, Serikali imeandaa utaratibu maalumu wa kutoa taarifa zinazohusu upatikanaji wa mikopo ili kusaidia wananchi, kitu ambacho hakikuwepo awali” alisema Bw. Mwaigaga
Alisema lengo la mkakati huo ni kumrahisishia mwananchi mwenye nia ya kuanzisha kiwanda kupata taarifa sahihi ikiwa ni pamoja na utaratibu mzima wa kupata mkopo ambao unaondoa usumbufu kwa walengwa ikiwa ni utekelezaji wa nia ya Serikali ya Awamu ya Tano ya kuifanya Tanzania kuwa nchi ya viwanda.
Mikakati mingine ya Serikali katika kukuza sekta ya viwanda nchini ni pamoja na kuanzisha programu ya kuendeleza viwanda vidogo vidogo katika mikoa ya Ruvuma, Pwani, Iringa, Tanga na Manyara.
Naye, Afisa Uchumi kutoka Wizara hiyo Bw. Vicent Turuka alisema katika kutekeleza azma ya Serikali ya kuifanya Tanzania kuwa nchi ya viwanda, Wizara inawaunganisha wafanyabiasha wadogo wadogo na wanunuzi wakuu na kuwapatia masoko ya mazao mfano zao la ufuta lina soko kwa kampuni ya Oramu pamoja na Murza Mills.
Aidha, wananchi wamesisitizwa kutembelea banda la Wizara ya Viwanda na Bishara  pamoja na taasisi zake za BRELA, TBS, TFDA , CBE na SIDO lililopo katika viwanja hivyo vya maonesho ili kupata taarifa mbalimbali kuhusu namna za kufanya biashara pamoja na kuanzisha viwanda nchini.

LESOTHO YAKUBALI KUTEKELEZA MASHARTI YA SADC

NAM1 
Waziri  Mkuu, Kassim Majaliwa akishiriki akatika Mkutano wa  Viongozi  Wakuu wa  Nchi  na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika ( SADC) uliofanyika kwenye hoteli ya Grand Palm  mjini Gaborone Botswana Juni 28. Waziri Mkuu alimwakilisha Rais John Pombe Magufuli kwenye mkutano huo. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
……………………………………………………………………………………………
WAZIRI MKUU wa Lesotho, Dk. Pakalitha Mosisili amekubali kutekeleza masharti yaliyowekwa na Wakuu wa Nchi na Serikali na Kamati ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Jumuiya ya Uchumi na Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC Double Troika Summit), na kuridhia timu ya uchunguzi kwenda nchini humo kufanya uchunguzi wa hali ya kiusalama na kisiasa.
Dk. Mosisili ametoa uamuzi huo leo (Jumanne, 28 Juni, 2016) wakati wa kikao maalum cha Wakuu wa Nchi na Serikali (SADC Summit) na wakuu wa nchi wanaounda Kamati ya Siasa, Ulinzi na Usalama (SADC Organ on Politics, Defense and Security Cooperation) kilichofanyika kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa (GICC), jijini Gaborone, Botswana.
Pia amekubali viongozi waupinzani na baadhi ya maofisa wa kijeshi wanaoishi uhamishoni ambao walikimbia machafuko yaliyotokea nchini humo warejee nchini mwao na kuahidi kwamba atahakikisha wanapatiwa ulinziwa kutosha.
Januari mwaka huu, mkutano wa SADC Double Troika uliagizakwambaifikapo Februari Mosi, mwaka huuSerikali ya Lesotho iwe imetangaza matokeo ya Tume iliyoundwa kuchunguza matatizo ya kisiasa na kiusalama nchini humo hususan mazingira yaliyopelekea kifo cha marehemu Luteni Jenerali Maaparankoe Mahao ambaye alikuwa Mkuuwa Majeshi.
Kwaupande wake, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ambaye alikuwa akimwakilisha Rais Dk. John Pombe Magufuli katika kikao hicho amesema wamepitia ripoti iliyoundwa na timu ya SADC iliyochunguza kuhusu matatizo ya Lethoto ambayo iliwahoji Viongozi wa Serikali, Jeshi, Bunge na familia ya marehemu Luteni Jenerali Mahao.
“Lengo la hatuahiiza SADC ni kuhakikisha inarejesha hali ya amani na utulivu kwenye maeneo ya siasa, ulinzi na usalama katika nchi wanachama wa Jumuiya hiyo ili wananchi wake waweze kuishi vizuri,” amesema
Pia Waziri Mkuu amesema Tanzania inatarajiwa kukabidhiwa uenyekiti wa Wakuu wa Nchina Serikali na Kamati ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Jumuiya ya Uchumi na Maendeleo ya nchi za Kusini mwa Afrika (SADC Double Troika Summit), Agosti mwaka huu ambapo kitafanyika kikao kingine nchini  Tanzania.
Mkutano huo wa ulifunguliwa na Rais wa Botswana, Mhe. Lt. Jen. Seretse Khama Ian Khama na ulihudhuriwa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ambaye alikuwa akimwakilisha Rais Dk. John Pombe Magufuli;  Rais wa Afrika Kusini, Bw. Jacob Zuma; Rais wa Msumbiji, Bw. Filipe Jacinto Nyusi; Rais wa Zimbabwe, Bw. Robert Mugabe, Mfalme Muswati wa III wa Swazland.
SADC Double Troika ni kikao maalum kinachojumuisha Wakuu wa Nchi na Serikali (SADC Summit) na wakuu wa nchi wanaounda Kamati ya Siasa, Ulinzi na Usalama (SADC Organ on Politics, Defense and Security Cooperation). 
SADC Double Troika ni mkutano unaohusisha viongozi wakuu watatu wanaoongoza chombo cha ushirikiano wa siasa, ulinzi na usalama na wengine watatu kutoka kwenye Mkutano wa wakuu wa nchi wanachama wa SADC. Hawa wanawakilisha mwenyekiti aliyepo madarakani, mwenyekiti aliyemaliza muda wake na mwenyekiti ajaye ambaye huwa ni makamu mwenyekiti.
Chini ya muundo wa SADC, kuna mambo makuu mawili; la kwanza likiwa ni utangamano wa kikanda ambao unasimamiwa na mkutano wa wakuu wa nchi (SADC Summit) na la pili ni la siasa, ulinzi na usalama ambalo linasimamiwa na chombo maalum (SADC Organ).
Wajumbe wa mkutano wa SADC Organ ni Msumbiji (Mwenyekiti); Afrika Kusini (Mwenyekiti aliyemaliza muda wake) na Tanzania inayotarajia kuchukua uenyekiti wa chombo hiki ifikapo Agosti, 2016. Botswana, Zimbabwe na Swaziland ndizo zinaunda SADC Summit.

TAARIFA YA UTEUZI KWA VYOMBO VYA HABARI

index 
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Mosses Nnauye amemteua Dkt. Herbert F. Makoye kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa).  Uteuzi huu umefanywa chini ya Kifungu Na. 9 (1) cha Sheria ya Wakala wa Serikali (Executive Agencies Act) iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2009 ambacho kinampa Waziri mamlaka ya kufanya uteuzi huo.  Uteuzi huu utaanza tarehe 01/07/2016.
Dkt. Makoye anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Bw. Juma Bakari aliyestaafu kwa mujibu wa Sheria ya Utumishi wa Umma. Dkt. Makoye mwenye Shahada ya Uzamivu (PhD) kutoka Chuo Kikuu cha Ghana na Shahada ya Umahiri – Sanaa (M. A in Theatre Arts) toka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
Kabla ya uteuzi huu Dkt. Makoye alikuwa Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu Dar es Salaam Idara ya Sanaa na Maonesho.
Imetolewa na,
Genofeva Matemu,
Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
WIZARA YA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO.
28 Juni,2016

Jumamosi, 25 Juni 2016

MR NICE ATOA ALBAM YAKE MPYA


WhatsApp-Image-20160624 (1)












   Msanii wa muziki nchini Mr nice ameachia ablam yake iitwayo KIOO siku ya jumatano huko nchini Kenya na mauzo yake kuwa makubwa kufikia nakala 5000.
Msanii huyo amesema kuwa kama alivyoahidi kutoa albamu tu na sio single tena kwani natembea kiutu uzima,na mpaka sasa ameuza nakala hizo 5000 katika nchi ya kenya tu hivyo bado nchi zingine pia.
   Mr Nice kwa sasa yupo nchini Kenya kwa ajili ya kuitangaza albamu yake mpya huku akifanya show mbalimbali na anategemea akimaliza nchini hapo ataelekea nchini Uganada.

SHILOLE AFUNGUA LABEL YAKE NA KUMSAINI MSANII CHIPUKIZI


11330616_296972493806688_1211325526_n
         Zuwena Mohamed "Shilole"

   Msanii wa muziki nchini Zuwena Mohamed almaarufu kwa jina la Shilole,ameanzisha label yake iitwayo Shilole Entertaiment,lakini pia kumsaini msanii chipukizi aitwae Amaselly.

   Shilole amefunguka kwa kusema ameamua kuanzisha label hiyo ili kuwasaidia wasanii ambao wana vipaji ila hawapati nafasi kwenye game
      Kwa upande wake msanii huyo Amaseiil a.k.a Gaucho,amesema kuwa alimshukuru shilole kwa uamuzi huo wa kumsainisha kwenye label yake hivyo anaahidi mambo mazuri katika game ya muziki.

Alhamisi, 23 Juni 2016

YANGA YATOA TAMKO KUHUSIANA NA MECHI YAO NA TP MAZEMBE


http://shaffihdauda.co.tz/wp-content/uploads/2016/06/IMG-20160623-WA0011.jpg

MASHINDANO YA KUSOMA QURAAN YA KIMATAIFA KUANZA KUTIMUA VUMBI LEO USIKU

   Jumuiya ya kuhifadhisha Quraan Tanzania imetangaza rasmi kuanza kwa mashindano ya kusoma Quraan ya kimataifa kuanzia leo usiku baada ya swala ya Tarawee katika msikiti wa mtoro jijini dar es salaam na kilele chake kuwa ni siku ya jumapili katika ukumbi wa Diamond Jubilee.
   Hayo yamesemwa na mwenyekiti wa jumuiya hiyo Shekhe Otham Ally Katoro wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jijini hapa na kutoa ufafanuzi wa mashindano hayo kwa ujumla wake.
   Aidha Shekhe Othman alisema kuwa kila nchi imetoa mshiriki mmoja na wote wamekariri juzuu zote thelathini za kitabu cha Quraan na washindikatika shindano hilo watazawaida pesa kuanzia dola 5000.
    Mashindano hayo yana jumla ya washiriki 22 na yataanza leo na kuendelea hadi siku ya jumapili  ambayo ndio kilele chake katika ukumbi wa Diamond Jubilee na mgeni rasmi siku hiyo ni waziri mkuu Mheshimiwa Kassim Majaliwa.

Jumatano, 22 Juni 2016

KUPATWA KWA JUA KIPETE KUNATARAJIA KUTOKEA TANZANIA

Chuo kikuu huria nchini Tanzania,kimetangaza tukio la kupatwa kwa jua kipete ambalo linatarajia kutokea septemba mosi mwaka huu,hivyo macho yote yataelekezwa nchini Tanzania ili kushuhudia tukio hilo.
Hayo yamezungumzwa na Dk Nooraj T Jiwaji ambaye ni mtaalam wa kitivo cha sayansi na teknolojia na elimu ya mazingira katika chuo hiko wakati akizungumza na wanahabari jijini dar es salaam.
Tukio ilo ambalo ni nadra sana kutokea hasa kwa kizazi hiki cha sasa ambalo huwa linatokea kila baada ya miaka 15,hivyo linatarajiwa kutokea septemba mosi na hivyo wananchi na jamii nzima kwa ujumla wataelekea Rujewa karibu kabisa na mkoa wa Mbeya,kusini mwa Tanzania kushuhudia duara la jua linavyobadilika kuwa pete ya jua.