Jumatano, 10 Agosti 2016

ITV,CLOUDS TV NA CLOUDS REDIO VYAPIGWA FAINI

Mamlaka ya Udhibiti wa Mawasiliano Tanzania (TCRA) imevipatia onyo na kuvipiga faini ya shiilingi milioni 19 vituo vya ITV na Clouds TV pamoja na  kimoja cha redio ambacho ni Clouds Fm kwa kosa la kukiuka maadili ya utangazaji.
Akitoa uamuzi huo uliofikiwa na Kamati ya Maudhui ya mamlaka hiyo Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Joseph Mapunda alisema kwamba vituo hivyo vilibainika kukiuka Kanuni na taratibu za Huduma ya Utangazaji na kuvitaka kuwa wawe wasimamizi wazuri wa vipindi vyao.

Mapunda aliendelea kwa kusema kamati hiyo imekipa onyo na kukipiga faini ya Sh milioni 10 kituo cha televisheni cha ITV kwa makosa mawili,kosa  la kwanza ni kupitia kipindi chake cha Kumekucha cha Juni 15, mwaka huu kilichoruka hewani kati ya saa 1:00 na 1:30 asubuhi ambacho mtangazaji alifanya mahojiano na Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa kuhusiana na  mwenendo wa Bunge la Bajeti, lakini Mchungaji Msigwa alitamka maneno ya kashfa dhidi ya Naibu Spika wa Bunge, Dk Tulia Ackson lakini mtangazaji hakuchukua hatua zozote za kumuomba Mheshimiwa Msigwa kufuta lugha ya matusi alioitumia.
Na kosa la pili,  kituo hicho kilikiuka kanuni katika taarifa ya habari ya Juni 23 kati ya saa 1:00 na 2:00 asubuhi, kilitangaza taarifa ya msichana wa miaka 16 aliyebakwa na kupewa ujauzito na walitumia utambulisho wa msichana huyo kwa jina na shule anayosoma.Na katika utetezi wake mwakilishi kutoka ITV,Steven Chuwa alikiri kuwa Mchungaji Msigwa alitoa maneno ya kashfa na hakutembea katika ahadi yake ya kutomkashifu mtu.

Aidha alisema kama mtangazaji angemuomba kufuta kauli, mjadala ungekuwa mkubwa zaidi Alisema watachukua hatua za kumwomba radhi Dk Tulia kutokana na kashfa hiyo.Kwa upande wa Kituo cha Clouds Tv, kituo hicho kimepewa onyo na kupigwa faini ya Sh milioni nne ambazo wanapaswa kulipa ndani ya siku 30 kuanzia siku ya hukumu.

Mapunda alisema kituo hicho kupitia kipindi chake cha Hip Hop, kilichorushwa kati ya saa 8:00 mchana na 12:00 jioni, kilirusha video ya nyimbo za Asanteni kwa Kuja wa Mwana FA na Break It Down wa Lil Bebbie, ambazo zinadhalilisha utu wa mwanamke.

Vile vile,Clouds Fm pia imepewa onyo na kupigwa faini ya Sh milioni tano kwa vipindi vyake vya ‘Power Breakfast’ na Jahazi kwa walikiuka kanuni za utangazaji.Na katika kipindi cha Jahazi cha Mei 9, kilichorushwa kati ya saa 10:00 hadi 12:55 jioni, watangazaji walisikika wakishabikia taarifa ya mtu kufanya ngono na mbuzi, ambako walieleza kuwa mtu huyo na mbuzi ni kama mtu na mpenzi wake, jambo lililoonesha wanahamasisha vitendo hivyo.

Aidha, Mei 18, mwaka huu katika kipindi cha Power Breakfast, kilichorushwa kati ya sa 12:00 na 4:00 asubuhi baada ya kusoma taarifa ya Hospitali ya Taifa Muhimbili kuhusu kupandikizwa kwa sehemu za siri za kiume kwa mtoto wa miaka mitatu, aliyezaliwa akiwa hana na kulelewa kama mtoto wa kike.

Jumamosi, 16 Julai 2016

BASATA KUUFUNGIA WIMBO WA PALE KATI WA MSANII NEY WA MITEGO




Baraza la Sanaa la Taifa nchini Tanzania  (BASATA) limeufungia rasmi wimbo wa msanii Ney wa mitego uitwao Pale kati kutokana na ukiukwaji mkubwa wa maadili ya kitanzania.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na Katibu Mtendaji wa BASATA, Godfrey Mngereza ameeleza kuwa msanii huyo amekuwa na tabia na mienendo yenye kuchafua sekta ya sanaa yeye binafsi kupitia kutoa kazi chafu na kufanya maonyesho yenye kukiuka maadili.

Alisema“Kazi zake zikikiuka maadili na kudhalilisha utu wa mwanamke sambamba na kutoa lugha za matusi na za kudhalilisha watu wa kada mbalimbali.'

Aidha aliongeza kwa kusema wao BASATA waliwahi kumuita msanii huyo mara kadhaa kutokana na tabia yake ya kutoa kazi zisizokuwa na maadili na aliahidi kubadilika na kuachana na tabia hiyo. Kwa hiyo kuendelea kwake kufanya matukio haya kwa makusudi ni uthibitisho kwamba hajabadilika na kwa maana hiyo ameendelea kuidhalilisha sanaa na wasanii wa kitanzania wenye kujitambua na kuiheshimu kazi ya sanaa kama kazi nyingine. Kwa sasa Msanii huyu ametoa wimbo mwingine wa ambao uko mitandaoni ukipambwa na picha chafu zinazoonesha mwanamke akiwa mtupu yaani uchi wa mnyama

RAISI MAGUFULI AFANYA UTEUZI MWINGINE

Leo tarehe 16 mwaka 2016 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk John Pombe Magufuli  amefanya uteuzi wa viongozi na watendaji wa taasisi mbalimbali za Serikali na pia amewapandisha vyeo maafisa wa Jeshi la Polisi Tanzania.
Uteuzi huo ni kama ifuatavyo;
1)Augustino Lyatonga Mrema.
⦁ Ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Taifa ya Parole kwa kipindi cha miaka mitatu, kuanzia leo tarehe 16 Julai, 2016.
⦁ Augustino Lyatonga Mrema anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Jaji Mstaafu Mhe. Eusebia Nicholaus Munuo ambaye muda wake umemalizika.
2)Prof. William R. Mahalu
⦁ Ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete. Uteuzi huu umeanza leo tarehe 16 Julai, 2016.
3Prof. Mohamed Janabi
⦁ Ameteuliwa kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete. Uteuzi huu umeanza tarehe 15 Julai, 2016.
4)Prof. Angelo Mtitu Mapunda
⦁ Ameteuliwa kuwa Kamishna wa Tume ya Utumishi wa Mahakama kwa kipindi cha miaka mitatu. Uteuzi huu umeanza tarehe 15 Julai, 2016.
 5)Sengiro Mulebya
⦁ Ameteuliwa kuwa Kamishna wa Tume ya Utumishi wa Mahakama kwa kipindi cha miaka mitatu. Uteuzi huu umeanza tarehe 15 Julai, 2016.
6)Oliva Joseph Mhaiki
⦁ Ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC). Uteuzi huu umeanza tarehe 15 Julai, 2016.
7)Winifrida Gaspar Rutaindurwa
⦁ Ameteuliwa kuwa Katibu wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC). Uteuzi huu umeanza tarehe 15 Julai, 2016.
8)Charles Rukiko Majinge
⦁ Ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya wadhamini ya Hospitali ya Taifa Muhimbili. Uteuzi huu umeanza leo tarehe 16 Julai, 2016.
9)Dkt. Julius David Mwaiselage
⦁ Ameteuliwa kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taasisi ya Saratani ya Ocean Road. Uteuzi huu umeanza tarehe 15 Julai, 2016.

Hali kadhalika Rais  Magufuli amewapandisha vyeo maafisa 25 wa Jeshi la Polisi kutoka cheo cha Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) na kuwa Naibu Kamishna wa Polisi (DCP).
Waliopandishwa vyeo hivyo ni kama ifuatavyo;
1)Essaka Ndege Mugasa
2)Adamson Afwilile Mponi
3)Charles Ndalahwa Julius Kenyela
4)Richard Malika Revocatus
5)Geofrey Yesaya Kamwela
6)Lucas John Mkondya
7)John Mondoka Gudaba
8)Matanga Renatus Mbushi
9)Frasser Rweyemamu Kashai
10)Ferdinand Elias Mtui
11)Germanus Yotham Muhume
12)Fulgence Clemence Ngonyani
13)Modestus Gasper Lyimo
14)Mboje John Shadrack Kanga
15)Gabriel G.A. Njau
16)Ahmed Zahor Msangi
17)Anthony Jonas Rutashubulugukwa
18)Dhahir Athuman Kidavashari
19)Ndalo Nicholus Shihango
20)Shaaban Mrai Hiki
21)Simon Thomas Chillery
22)Leonard Lwabuzara Paul
23)Ahmada Abdalla Khamis
24)Aziz Juma Mohamed
25)Juma Yussuf Ally

Vilevile, Rais  John Pombe Magufuli amewapandisha vyeo maafisa wa Jeshi la Polisi wengine 34 kutoka cheo cha Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) na kuwa Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP)kuanzia july 15 mwaka huu.

Waliopandishwa vyeo hivyo ni kama ifuatavyo;
1)Fortunatus Media Musilimu
2)Goyayi Mabula Goyayi
3)Gabriel Joseph Mukungu
4)Ally Omary Ally
5)Edward Selestine Bukombe
6)Sifael Anase Mkonyi
7)Naftari J. Mantamba
8)Onesmo Manase Lyanga
9)Paul Tresphory Kasabago
10)Dadid Mshahara Hiza
11)Robert Mayala
12)Lazaro Benedict Mambosasa
13)Camilius M. Wambura
14)Mihayo Kagoro Msikhela
15)Ramadhani Athumani Mungi
16)Henry Mwaibambe Sikoki
17)Renata Michael Mzinga
18)Suzan Salome Kaganda
19)Neema M. Mwanga
20)Mponjoli Lotson
21)Benedict Michael Wakulyamba
22)Wilbroad William Mtafungwa
23)Gemini Sebastian Mushi
24)Peter Charles Kakamba
25)Ramadhan Ng’anzi Hassan
26)Christopher Cyprian Fuime
27)Charles Philip Ulaya
28)Gilles Bilabaye Muroto
29)Mwamini Marco Lwantale
30)Allute Yusufu Makita
31)Kheriyangu Mgeni Khamis
32)Nassor Ali Mohammed 
33)Salehe Mohamed Salehe
34)Mohamed Sheikhan Mohamed

Jumanne, 12 Julai 2016

RAISI MAGUFULI AAGIZA VYOMBO VYA SERIKALI KUTUMIA MASHINE ZA EFD

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dk John Pombe Magufuli amewaagiza makatibu wakuu kuhakikisha vyombo vyote vinavyokusanya mapato serikalini vinatumia mashine za kielekrtoniki (EFD).
 
Rais Magufuli ameyasema hayo wakati akizungumza na wakurugenzi wateule wa Halmashauri,Wilaya,Majiji na Manispaa Ikulu jijini Dar es Salaam wakati wa kiapo cha ahadi ya uadilifu kwa viongozi hao wa umma.
 
“Vyombo vya Serikali lazima vianze kutumia mashine za EFD,haiwezekani  wafanyabiashara wawe na mashine za EFD alafu maafisa wa serikali hawana,kama tumeamua kwenda kwa elektroniki lazima twende hivyo”Alisema Rais Magufuli.
 
Aidha amewataka wakurugenzi  wote kuchukua mashine hizi na kwenda nazo katika maeneo yao ya kazi ili ziwasaidie katika ukusanyaji wa mapato ya serikali katika halmshauri zao.
 
Hali kadhalika amewaagiza wakurugenzi hao kukusanya kodi na kutatua kero za wananchi wa chini zisizokuwa na lazima na kuongezea kuwa kama watakuta watendaji wa chini yao wasioendana  na kasi ya awamu ya tano basi watumie madaraka yao kuwaweka sawa.
  .
 
Aidha Rais magufuli amewataka wakurugenzi hao kusimamia kuanzishwa kwa viwanda vidogo vidogo katika maeneo yao ili kukamilisha azma ya serikali ya awamu ya tano ya kuwa na viwanda.


ETHIOPIA YAZIMA MITANDAO YA KIJAMII

Waethiopia waliamka Wikiendi wakajikuta hawana huduma hizo za mitandao ya kijamii kama Facebook, Twitter, Instagram na Viber ambapo Serikali imefunga mitandao hiyo tangu Jumamosi usiku.

Msemaji wa serikali ameiambia shirika la habari la AFP kuwa serikali ilichukua hatua hiyo kama njia ya kuzuia wanafunzi wasivurugwe na ushawishi wa mitandao hiyo ya kijami na hatua hiyo imetokea majuma kadhaa baada ya baadhi ya makaratasi ya mitihani kuchapishwa kwenye mitandao ya kijamii na kulazimu serikali kufutilia mbali mitihani hiyo iliyodukuliwa.''Serikali imechukua hatua hiyo kwa muda hadi siku ya Jumatano.

Tumegundua kuwa mitandao ya kijamii huvuruga kabisa ratiba ya vijana na haswa wanafunzi'', alisema msemaji wa serikali Getachew RedaSerikali imechukua hatua hiyo kwa muda hadi siku ya Jumatano mitihani itakapokuwa imekamilika

Hatu hiyo  ya kuifungia mitandao ya kijamii kama facebook,twitter na Instagram bila shaka imewaudhi wanaharakati wa kupigania uhuru wa habari nchini Ethiopia.