Jumanne, 12 Julai 2016

ETHIOPIA YAZIMA MITANDAO YA KIJAMII

Waethiopia waliamka Wikiendi wakajikuta hawana huduma hizo za mitandao ya kijamii kama Facebook, Twitter, Instagram na Viber ambapo Serikali imefunga mitandao hiyo tangu Jumamosi usiku.

Msemaji wa serikali ameiambia shirika la habari la AFP kuwa serikali ilichukua hatua hiyo kama njia ya kuzuia wanafunzi wasivurugwe na ushawishi wa mitandao hiyo ya kijami na hatua hiyo imetokea majuma kadhaa baada ya baadhi ya makaratasi ya mitihani kuchapishwa kwenye mitandao ya kijamii na kulazimu serikali kufutilia mbali mitihani hiyo iliyodukuliwa.''Serikali imechukua hatua hiyo kwa muda hadi siku ya Jumatano.

Tumegundua kuwa mitandao ya kijamii huvuruga kabisa ratiba ya vijana na haswa wanafunzi'', alisema msemaji wa serikali Getachew RedaSerikali imechukua hatua hiyo kwa muda hadi siku ya Jumatano mitihani itakapokuwa imekamilika

Hatu hiyo  ya kuifungia mitandao ya kijamii kama facebook,twitter na Instagram bila shaka imewaudhi wanaharakati wa kupigania uhuru wa habari nchini Ethiopia.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni