Jumatatu, 4 Julai 2016

Taasisi ya maridhiano Tanzania ambayo inaundwa na madhehebu ya dini tofauti tofauti nchini,imejitambulisha rasmi kwa jamii pamoja na kueleza kazi zao wanazozifanya katika taasisi hiyo.
Aidha taasisi hiyo itafanya shughuli ya uzinduzi wa taasisi hiyo siku ya 13/07/2016 katika ukumbi wa Karimjee jijini dar es salaam,kuanzia saa kumi jioni hadi saa moja na nusu jioni na mgeni rasmi katika uzinduzi huo atakua waziri wa mambo ya ndani Mheshimiwa Mwigulu Nchemba.
Vilevile shughuli hizo zitaambatana na utoaji wa Tuzo kwa watu mbalimbali ambao wamechangia kudumisha amani na watu hao ni kama wafuatao:Mama Maria Nyerere,Jakaya Mrisho Kikwete,IGP Saidi Mwema,Reginald Mengi,Mustafa Sabodo,Helen Simba,Sadick Meck Sadick,Ruge Mutahaba,Albert Sanga(mwanzilishi wa bunge la uchumi nchini).

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni