Jumanne, 5 Julai 2016

TFDA YATOA RAI KWA JAMII IWE INATOA TAAARIFA JUU YA MATUMIZI YA DAWA

   Mamlaka ya chakula na dawa nchini (TFDA),imetoa rai kwa wataalam wa afya na wananchi kwa ujumla kutoa taarifa juu ya madhara yoyote yatokanayo na matumizi ya dawa kwa kutumia mfumo mpya wa kieletroniki unaotumia computer na smartphone.
   Hayo yamesemwa na meneja mawasiliano wa mamlaka hiyo bi Gaudensia Mwisenza alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari juu ya masuala mazima ya utoaji taarifa na kufafanua zaidi majukumu yao.
  Aidha Afisa wa kitengo cha usalama wa majaribio ya dawa katika mamlaka hiyo Dr Alex Kayamba alielza jinsi ya kutumia mfumo huo wa kieletroniki kwa kuingia internet na kwa wale ambao hawana smart phone wanaangalia ni jinsi gani wanaweza kufanya ili nao waweze kutoa taarifa kama wengine kwani kwa sasa mfumo huo upo kwenye majaribio na haujazinduliwa rasmi kabisa.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni