Alhamisi, 7 Julai 2016

IKULU YATOA TAARIFA YA MAREKEBISHO

Taarifa kutokea Ikulu nchini Tanzania, inasema kwamba kuna marekebisho madogo katika majina yaliyopo kwenye orodha ya wakurugenzi wa Halmashauri za Majiji, Manispaa, Miji na Wilaya iliyotolewa hapo awali ambapo Dkt. Leonard Moses Massale ametangazwa kuwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Dodoma.

Taarifa hiyo inasema kwamba Jina hilo limeingizwa katika Orodha ya Wakurugenzi wa halmashauri kwa makosa na kwa sababu hiyo Dkt. Leonard Moses Massale anaendelea kuwa Mkuu wa wilaya ya Ilemela Mkoani Mwanza. Kufuatia marekebisho hayo, uteuzi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma utatangazwa  hapo baadaye.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni