Chuo kikuu huria nchini Tanzania,kimetangaza tukio la kupatwa kwa jua kipete ambalo linatarajia kutokea septemba mosi mwaka huu,hivyo macho yote yataelekezwa nchini Tanzania ili kushuhudia tukio hilo.
Hayo yamezungumzwa na Dk Nooraj T Jiwaji ambaye ni mtaalam wa kitivo cha sayansi na teknolojia na elimu ya mazingira katika chuo hiko wakati akizungumza na wanahabari jijini dar es salaam.
Tukio ilo ambalo ni nadra sana kutokea hasa kwa kizazi hiki cha sasa ambalo huwa linatokea kila baada ya miaka 15,hivyo linatarajiwa kutokea septemba mosi na hivyo wananchi na jamii nzima kwa ujumla wataelekea Rujewa karibu kabisa na mkoa wa Mbeya,kusini mwa Tanzania kushuhudia duara la jua linavyobadilika kuwa pete ya jua.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni